Simiyu; Tarehe 04/08/2020
Wananchi mbalimbali katika mkoa wa Simiyu wametembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili kupata elimu ya hali ya hewa inayotolewa na wataalam kutoka Mamlaka. Akizungumza wakati na wananchi hao kwa nyakati tofauti tofauti, Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, alisema TMA ni taasisi yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi hususan katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.
“Basi mwananchi tunakuomba utumie taarifa zetu za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli zetu za kimaendeleo, na katika azma nzima ya kuifanya nchi yetu kuwa nchi ya viwanda”. Alisema Dkt. Chang’a.
Aidha, aliendelea kusisitiza kuwa matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa ni chachu kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi, huku akisisitiza wananchi kuchagua vingozi bora kwa maendeleo ya nchi yetu ambayo tayari imefikia uchumi wa kati.
Kwa upande wa Meneja wa Kanda ya Ziwa-TMA, Ndg. Augustine
Nduganda aliwakaribisha wananchi wa Kanda ya Ziwa hususan Mashariki, kutembelea
banda la TMA ili waweze kupata elimu ya sayansi ya hali ya hewa kwa ujumla
ikiwa ni pamoja na kujionea vifaa vya hali ya hewa, jinsi uangazi, uchambuzi na
utayarishaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwemo utabiri unavyofanyika na pia
kupata elimu kuhusus mabadiliko ya hali ya hewa.